




============================================================================================================
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Timu ya wataalamu kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) inayosimamia Mradi wa Kudhibiti Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu (EHPMP) ofisini kwake jijini Dodoma leo Februari 01, 2026.
Wakiongozwa na Mratibu wa mradi huo Mhandishi Dkt. Befrina Igulu wakiwa na timu ya wataalamu kutoka Benki ya Dunia wamekutana na Dkt Muyungi kwa lengo la kutathmini uendelevu wa mradi na kuhakikisha uzingatiaji wa mikataba ya kimataifa.
Majadiliano yaligusia upatikanaji wa rasilimali fedha za ziada kwa ajili ya usimamizi wa taka za kielektroniki ambazo zina uhusiano wa karibu na athari za madini joto kama zebaki.
Aidha, Benki ya Dunia wamepongeza hatua zilizofikiwa katika kutimiza malengo ya msingi ya utekelezaji wa mradi huu.