Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu Rasmi ya Ofisi ya Makamu wa Rais

Dkt. Muyungi, NEMC, Benki ya Dunia wajadiliana kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo
Feb 03, 2026
Dkt. Muyungi, NEMC, Benki ya Dunia wajadiliana kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akizungumza na Ujumbe kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) pamoja na Benki ya Dunia kuhusu kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wakati wa kakao kilichofanyika jijini Dodoma.
Na Robert Hokororo

============================================================================================================

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Timu ya wataalamu kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) inayosimamia Mradi wa Kudhibiti Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu (EHPMP) ofisini kwake jijini Dodoma leo Februari 01, 2026. 

Wakiongozwa na Mratibu wa mradi huo Mhandishi Dkt. Befrina Igulu wakiwa na timu ya wataalamu kutoka Benki ya Dunia wamekutana na Dkt Muyungi kwa lengo la kutathmini uendelevu wa mradi na kuhakikisha uzingatiaji wa mikataba ya kimataifa.

Majadiliano yaligusia upatikanaji wa rasilimali fedha za ziada kwa ajili ya usimamizi wa taka za kielektroniki ambazo zina uhusiano wa karibu na athari za madini joto kama zebaki.

Aidha, Benki ya Dunia wamepongeza hatua zilizofikiwa katika kutimiza malengo ya msingi ya utekelezaji wa mradi huu.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi