




=======================================================================================================================
Watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wameshiriki mazoezi ya pamoja yaliyofanyika leo, Julai 11, 2026, katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha afya njema, ustawi wa watumishi na kuimarisha mshikamano mahali pa kazi.
Mazoezi hayo yanadhihirisha umuhimu wa kuzingatia afya ya mwili na akili kama msingi wa kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya utumishi wa umma.