Makamu wa Rais ashiriki uzinduzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere
Aug 22, 2026
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki katika uzinduzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2115 katika eneo la Rufiji mkoani Pwani, leo tarehe 22 Agosti 2026.
Uzinduzi huo umeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri Mhe. Dkt. Mostafa Kamal Madbouly, Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina, Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi.
Na
Robert Hokororo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki katika uzinduzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP)