
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa (kushoto) na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (nyuma kulia) wakishiriki Semina Elekezi kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, iliyofunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Semina hiyo imefanyika leo Julai 28, 2026, Ikulu ndogo, Tunguu, Zanzibar, ikiwa na mada kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini.