Wananchi mbalimbali leo, Agosti 2, 2026, wameendelea kutembelea Banda la Ofisi ya Makamu wa Rais katika Viwanja vya Maonesho ya Nane Nane, Dodoma, kujionea na kujifunza kuhusu masuala ya mazingira, Muungano na uchumi wa buluu, pamoja na huduma na mafanikio yanayotekelezwa na Ofisi hiyo. Hii ni siku ya pili tangu maonesho hayo yafunguliwe rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba.
Read More