Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Chande akizungumza na mabalozi wa mazingira wakati akifungua Warsha kwa mabalozi hao kuhusu utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga akitoa neno la ukaribisho wakati wa Warsha kwa mabalozi hao kuhusu utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya mabalozi wa mazingira wakiwa katika Warsha kuhusu utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Mohammed Khamis Abdulla akifuatilia Warsha ya mabalozi wa mazingira kuhusu utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Andrew Komba akifuatilia Warsha ya mabalozi wa mazingira kuhusu utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Chande (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na mabalozi wa mazingira baada ya kufungua Warsha kwa mabalozi hao kuhusu Novemba 16, 2021 jijini Dar es Salaam.

============================================================================

Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Chande ametoa wito kwa mabalozi wa mazingira nchini kuhakikisha wanasaidia kudhibiti uharibifu wa mazingira ili vizazi vijavyo viweze kukuta nchi ikiwa na mazingira mazuri.

Chande ametoa wito huo Novemba 16, 2021 wakati akifungua Warsha kwa mabalozi hao ikilenga utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa Serikali imewaamini na kuwapa ubalozi ili waisaidie jamii kuweza kuishi kwa amani bila ya taharuki inayosababishwa na uharibifu wa mazingira.

“Tanzania tuna ulazima wa kulinda mazingira, tusifike wakati tukawadhurumu watoto wetu ambao hata hawajazaliwa hii ni dhambi kubwa kwani hata wasomi wanasema mnusuru ndugu yako anayedhurumiwa na anayedhurumu ndio kazi ya mabalozi.

“Niwaombe tutetee vizazi vinavyozaliwa miaka inayokuja wasipate dhuluma ya kuharibiwa mazingira na hivi karibuni tukiwa kwenye ziara mikoani tumeshuhudia karibu asilimi 60 mpaka 70 ya ardhi zimeharibiwa, sasa mabalozi tusaidie hili,” alisisitiza Chande.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Chande (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na mabalozi wa mazingira baada ya kufungua Warsha kwa mabalozi hao kuhusu Novemba 16, 2021 jijini Dar es Salaama utekelezaji wa Kampeni kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *