Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akishiriki katika zoezi la usafi wa mwisho wa mwezi katika Soko la Bonanza jijini Dodoma pamoja na wafanyabiashara katika soko hilo leo Julai 30, 2022 na kusisitiza agenda ya usafi wa mazingira kuwa endelevu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akibeba taka na kuzipeleka katika vyombo maalumu vya kuhifadhi taka mara baada ya kushiriki katika zoezi la usafi wa mwisho wa mwezi katika Soko la Bonanza jijini Dodoma pamoja na wafanyabiashara katika soko hilo leo Julai 30, 2022.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisukuma mkokoteni uliobeba taka  kuelekea  katika vyombo maalumu vya kuhifadhi taka kabla ya kusafirishwa kwenda Dampo mara baada ya kushiriki katika zoezi la usafi wa mwisho wa mwezi katika Soko la Bonanza jijini Dodoma pamoja na wafanyabiashara katika soko hilo leo Julai 30, 2022.
Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza na wafanyabiashara katika Soko la Bonanza jijini Dodoma mara baada ya kukamilika kwa zoezi la usafi katika soko hilo leo tarehe 30 Julai 2022.

==================================================================

Akiwa sokoni hapo amezungumza na wafanyabiashara na kutoa rai kwao kudumisha kwa vitendo kampeni ya usafi na mazingira kwa ujumla.

“Ndugu zangu agenda ya mazingira ni endelevu sote yatupasa kuitekeleza kwa vitendo na uwe ni utamaduni wetu sote” Dkt. Jafo alisisitiza.

Pia, amewapongeza wafanyabiashara sokoni hapo, mabalozi wa mazingira na wananchi kwa ujumla kwa kujitokeza kushiriki kufanya usafi wa mazingira

Amemwelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) ndani ya kipindi cha siku 14 kuhakikisha anafanya ukarabati wa mfumo wa maji taka katika soko hilo ili kuondoa adha inayowakumba wafanyabiashara kwa sasa.

“Ukarabati huu wa Mfumo wa maji taka katika eneo hili ufanyike mara moja, Mkurugenzi wa DUWASA asimamie kwa karibu utekelezaji wake” Alisisitiza Dkt. Jafo.

Aidha, Waziri Jafo alisema kuwa Serikali inatarajia kuzindua Kampeni ya usafi wa mazingira itakayofahamika kama ‘My Dustbin’ kwenye mitaa ya mbalimbali nchi nzima.

Alisema kampeni hiyo itasaidia kuweka mitaa katika hali ya usafi kwa kuwa kila mwananchi anatakiwa kutupa taka kwenye mapipa yaliyoyopo kwenye mitaa badala ya kutupa ovyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu wa Jiji la Dodoma Bw. Dickson Kimaro alisema wamekuwa wakihamasisha wananchi kushiriki usafi wa mazingira ili kuweka jiji katika hali ya usafi. Bw Kimaro alilisitiza uwajibikaji wa kila mwananchi katika kuhakikisha usafi unafanyika Mita tano kuzunguka maeneo ya Makazi  na Biashara. 

Alisema katika soko hilo wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla wamekuwa wakijitokeza kushiriki katika kufanya usafi wa mazingira sokoni hapo hivyo kuliweka jiji katika hali ya usafi.

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *