Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) inashirkiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) katika kutekeleza program na miradi mbalimbali ya hifadhi na usimamizi wa mazingira inayotekelezwa chini ya mikataba ya kimataifa.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akijibu maswali bungeni jijini Dodoma leo Septemba 13, 2022.

Katika swali la msingi Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Maryam Azan Mwinyi alitaka kufahamu Serikali ina mkakati gani wa kuunda kikosi kazi kuratibu Mikataba ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi kati ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Mhe. Khamis alisema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa Mikataba mbalimbali ya kimataifa ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ambayo inaratibiwa chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Aliongeza kuwa utaratibu unaotumika katika kuratibu masuala ya mikataba ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi kwa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo naibu waziri huyo alifafanua kuwa utaratibu huo ni wa kushirikiana katika majadiliano, pamoja na kushiriki katika mikutano ya kimataifa na utekelezaji wa mikataba hiyo.

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *