Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Khamis Hamza Khamis (kulia) akisalimiana na Bi. Janet Rogan mjumbe kutoka Serikali ya Uingereza katika Mkutano wa 27 wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Sharm El-Sheikh, Misri. Katika kikao hicho Tanzania na Uingereza zimekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya nchi mbili.